Revision 880043 of "Elgon (mlima)" on swwiki{{mergefrom|Mlima Elgon}}
[[Image:Mount elgon topo.jpg|thumb|250px|Eneo la Mlima Elgon]]
'''Mlima Elgon''' ni [[volkeno]] inayolala mpakani wa [[Uganda]] na [[Kenya]]. [[Kasoko]] yake ina kipenyo cha [[kilomita]] nane.
Elgon ni mlima mkubwa wa pili nchini Kenya baada ya [[Mlima Kenya]]. Upande wa Uganda ni mlima mkubwa wa mashariki ya nchi lakini milima ya [[safu ya Ruwenzori]] ni kubwa kushinda Elgon.
Jina la mlima limetokana na [[Waelgonyi]] walioishi upande wa kusini wa mlima. [[Wamaasai]] hutumia jina "Ol Doinyo Ilgoon" na upande wa Uganda huitwa "Masawa".
Kuna vilele vitano:
* ''Wagagai'' (4,321 m), upande wa Uganda
* ''Sudek'' (4,302 m), upande wa Kenya
* ''Koitobos'' (4,222 m), upande wa Kenya
* ''Mubiyi'' (4,211 m), upande wa Kenya
* ''Masaba'' (4,161 m), upande wa Kenya
Mito ya [[Suam (mto)|Suam]], [[Nzoia (mto)|Nzoia]] na [[Turkwel (mto)|Turkwell]] ina chanzo kwa mlima huu.
Vilele vya mlima ni sehemu ya hifadhi ya taifa pande zote mbili za Uganda na Kenya.
Miji ya karibu ni [[Kitale]], [[Bungoma]] na [[Webuye]] upande wa Kenya, halafu [[Tororo]] na [[Mbale]] upande wa Uganda.
{{Mbegu-jio-Uganda}}
[[Jamii:Milima ya Uganda|Elgon]]
[[Jamii:Milima ya Kenya|Elgon]]
[[Jamii:Volkeno za Afrika]]All content in the above text box is licensed under the Creative Commons Attribution-ShareAlike license Version 4 and was originally sourced from https://sw.wikipedia.org/w/index.php?oldid=880043.
![]() ![]() This site is not affiliated with or endorsed in any way by the Wikimedia Foundation or any of its affiliates. In fact, we fucking despise them.
|